lyrics



Fid-q-siri-ya-mchezo

Tuanze Na Lyrics Kabla Ya Link … ‘ Siri Ya Mchezo ‘ Ya Rapper Fid Q …

October 18, 2013 / by / 0 Comment Leo tulipaswa kukutana na season mpya ya Fidstyle Friday  lakini badala yake … CEO wa Cheusidawa ameamua kutupa ile #SiriYaMchezo mzima …
Siri Ya Mchezo ndio jina la ngoma mpya toka kwa #ToRe ya Top of Rap’s Elite a k a Fareed Kubanda A.K.A Fid Q …  ndani ya ngoma hii Fid Q ameonyesha uwezo wa juu kabisa kiuandishi kiasi cha kuacha gumzo mitandaoni baada ya kuitambulisha ngoma yake ndani ya xxl kwa dakika kumi leo mjengoni

.
Ngoma hiyo amemshirikishwa gwiji kutoka maandishi matatu yaani TMK,  Alwatan Juma Nature  a k a RAMBO ambaye amekitendea haki kiitikio kwa sauti yake tuliyoimiss kwa muda mrefu.
Uongozi mzima wa Cheusidawa umeonelea ni vyema kutanguliza Lyrics za ngoma hii ambayo link yake inasubiriwa kwa hamu na watu wote (ukiwemo wewe unayesoma habari hii hivi sasa) ili mpate kuikariri mapema kabla hamjasikia jinsi Fid Q alivyoichakaza juu ya beat …


                                                   Siri Ya Mchezo
Nilipotoka mbali na ninaheshimu nilipo/sikuwa na  umuhimu kihivyo… stimu  zikanipa elimu ya Biko/ Kimaandiko… kimistari.. hadi fans wanascream nikirap../  sikuamini kama nina zali mpaka nilipoidream hiphop/
Wanapagawa…. Na baadhi ya mambo nayoyajua.. pia nina uwezo wa kufanya mpaka madawa yanaugua/
 Wanapagawa na nyimbo ngumu hawa  #teamMabiiitoz  /
Achana na  power window.. sijui  rimz za dimpoz/  
haileti bingo, mshiko?  Star ishi simple/   sanaa iko hivyo sometimes.. hukataa kukaaa ulipo/
wanaodharau.. hujiletea matatizo..hawajui  kama wadau… hupendelea kukuona hivyo?/ bonge la staa.. donge la njaa.. hauna kitu/
 jikombe ugongwe…mtaaa  ukuone hauna ishu/
 ukishindwa kujiandaa… jiandae kushindwa/mjinga utaachwa unashangaa kumuona Martin Kadinda/ Usmati anaotinga, majumba mandinga ya bwana Almasi.. je hizi track za  harakati ni ujinga?/
HAPANA…. nguvu ya mamba ni maji/  na umaarufu au kutamba.. kushika namba ni bahati..sio kipaji  kama  Kubanda eti unachana kigumu/  kisa  track ikivuma sana kwenye chati  haidumu /
Amani kwa chachage na MAKUWADI wa SOKO HURIA../  baba asante kwa UTAFITI na ZAWADI ya ALMASI ya BANDIA/NYUMBANI… nasikiliza DUNIA YA SASA ya MARIJANI../  najiuliza tutarithi nini ikiwa IMANI ishakwisha tangu zamani?/ labda kubisha na wakinitisha najihami../  inasikitisha unapoibiwa na aliyekupigisha ni jirani/
‘’ Pole MAPROSOO’’ ( uhujumu –uchumi ) umefanya umetubu.. / WAZEE ni  wahuni  hadi soo waay back before SUGU/
Taifa la kondoo.. huendeshwa na serikali ya Dubu/ na MBWA MWITU wenye siri.. ili bepari umuabudu/ kimahakama, kiserikali, kidini umsujudu../  huo ni utumwa pia/Unafanya  vijana  wanaumia../   Tunaishia kufia mabatani kama nzi ndani ya glass ya bia..


CHORUS:  ( Juma Nature )
Siri ya mtungi aijuaye kata../ komaa… kaza.. kisha utapata/ x 2
Siri ya mchezo naijua  mimi.. tu.. na hakuna mwingine x 2


VERSE 2:
Tofauti ya BIASHARA na SIASA ikila hasara inaweza buma/ wakati SIASA kila mara ukiwa unang’ara ujue kuna.. kinara/ anayeunda msafara wa wanaojituma na kuchuma kwa kukufanya uwe imara hapo hasara hakuna/ KIDUMU CHAMA CHA MASELA… Ukoloni mambo leo umetupa uhuru wa bendera,/
 tuone kufuru za wenye hela/
TANZANIA ni ‘  demu wa mtungo ‘ wanamuiita CHA WOOTE/’’ HANGOVER .. ‘’anaikimbia kwa kupiga ‘ “ mtungi “ saa zote /Mkubwa anazuga atasolve… matatizo ya nchi yake/ ‘’na  gari bovu..’’  halisukumwi kwa kukaa ndani yake/ MAENDELEO ni ile ndoto..MWEZEKAJI ashaipuuza../  je  Kukaa karibu na moto ni kuuota au kujiunguza? / hakuna UHURU wa kweli (Africa) msidanganywe na illusion/ na daily tunafeli sababu ya  POLITICAL institutions/
CIVILIZATION  imeadvance sasa wanatuua economically../  hakuna utumwa mbaya kama ule wa kujiona uko free/ Kuusaka ukweli  ni  sawa na kumenya kitunguu/ kila ganda litakutoa machozi na utabaki macho juu/Ukishafika kwenye kiini  niambie nini utagundua..? zaidi ya mafaili yaliyounganika utaghairi kuyafunua?
Wamejivisha U-NOAH.. SAFINA zao zikatoboka/
Wakajivisha U-MUSSA.. FIMBO zao hazikugeuka NYOKA/
Sasa wanaujaribu U-MUNGU MTU kuamua nani leo atatoka….!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!???????????????????

No comments:

Post a Comment